Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa
Wadau Waalikwa Kutoa Maoni Yatakayofanyiwa Kazi na Kikosi Kazi cha Mhe. Rais Kuhusu Masuala ya Demokrasia Nchini
Vyama vya Siasa nchini vya ahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ambazo zinaongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan na Dkt. Hussen Ally Mwinyi, mtawalia.
Vyama vya Siasa ambavyo vinatarajia kushirikiana wakati wa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka huu bila kufuata Sheria ya Vyama vya Siasa kama ilivyoainishwa kwenye Kifungu Na.11 (a) cha Sheria hiyo vitakuwa vimevunja sheria.
Serikali inawaonya Wanasiasa kuacha propaganda za kupindisha ukweli na kutoa tafsiri potofu kuhusu Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 2018 kwa lengo la kuuhadaa umma kukataa muswada bali watumie fursa hii baada ya kuusoma , kutoa maoni yao stahiki kwa lengo la kuuboresha
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Mhe. Jaji Francis S.K Mutungi anawataarifu wajumbe wote wa Baraza la Vyama vya Siasa kuwa kikao cha Baraza la Vyama vya siasa kilichokuwa kimepangwa kufanyika tarehe 21 na 22 Desemba, 2018 mjini Zanzibar, kimeahirishwa.
Kikao cha Kamati ya Uongozi ya Baraza la Vyama vya Siasa kimefanyika leo Disemba 4, 2018 katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa Jijini Dar es Salaam, ikiwa ni maandalizi ya kikao cha Baraza la Vyama vya Siasa kinachotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi huu.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Katiba, Utumishi wa Umma na Utawala Bora kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Haruna Suleman amesema kuwa Suala la kusimamia vyama vya siasa nchini linahitaji umakini na usimamizi wa hali ya juu ikiwa ni njia bora ya kukuza democrasia na utawala bora nchini.
Maafisa wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa wanaojiandaa kushiriki katika uangalizi wa kampeni za uchaguzi unaotegemea kufanyika Decemba 2 mwaka huu, wameaswa kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa Sheria ili kujikita katika kuhudumia Vyama vyote kwa usawa.