• English
  • Staff Mail
  • Maswali
  • Wasiliana Nasi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa

  • Kuhusu sisi
    • Mamlaka
    • Dira
    • Majukumu
    • Muundo
    • Uongozi
    • Historia
  • Shughuli za Ofisi
    • Usajili wa Vyama
    • Uratibu wa Vyama
    • Ufuatiliaji wa Vyama
    • Gharama za Uchaguzi
    • Ruzuku ya Vyama
    • Utatuzi wa Migogoro
    • Taarifa za Vyama vya Siasa
  • Vyama vya Siasa
    • Usajili wa Kudumu
    • Usajili wa Muda
    • Orodha ya Vyama Vya Siasa
    • Baraza la Vyama
  • Sheria na Machapisho
    • Katiba
    • Sera
    • Sheria
    • Kanuni
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu EE
    • Fomu PP
    • Fomu za Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Matangazo
    • Mikutano
    • Warsha
    • Nafasi za kazi
    • Zabuni
  • Ziara
    • Taratibu za Ziara
    • Fomu ya Maombi
    • Utimilifu na Makatazo
    • Maoni ya Watembeleaji

Wadau Waalikwa Kutoa Maoni Kikosi Kazi cha Rais

Na: Mandishi Wetu – ORPP

Wadau wakaribishwa kutoa maoni,nyaraka na michango mbalimbali itakayotumika kufanya maboresho katika maeneo tisa yaliyobainishwa na Kikosi Kazi kilichokuwa kikipitia na kuchambua maoni yaliyotokana na mkutano wa wadau wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini uliofanyika tarehe 15, 16 na 17 Desemba 2021 jijini Dodoma.

Hayo yamebainishwa na Katibu wa Kikosi Kazi hicho Ndugu. Sisty Nyahoza kupita taarifa kwa umma iliyotolewa jana tarehe 14 April 2022 ambapo wadau wanaarifiwa kuanza kwa mchakato wa kupokea na kuwasilisha maoni yao kwa kikosi kazi hicho ndani ya siku 31 tangu kutolewa kwa taarifa hii.

Wito huo umekuja ikiwa ni baada ya Kikosi kazi hicho kilichoanza kazi rasmi tarehe 11 Januari 2022 ya kupitia na kuchambua maoni na mapendekezo yote yaliyotolewa na washiriki wa mkutano wa wadau na baadaye kikaainisha maeneo tisa mahususi ya kufanyia kazi kwa ustawi wa demokrasia nchini.

“Ili Kikosi Kazi kiweze kutekeleza kazi zake kwa mujibu wa mpango Kazi uliopo, mnaombwa kuwasilisha maoni, mapendekezo au nyaraka hizo, ndani ya muda wa siku thelathini na moja (31) kuanzia tarehe ya leo 14 Aprili 2022.” Ilisisitiza sehemu ya taarifa hiyo.

Taarifa hiyo imeyabainisha maeneo hayo kuwa ni pamaoja na; mikutano ya hadhara na ndani ya vyama vya siasa, masuala yanayohusu uchaguzi, mfumo wa maridhiano ili kudumisha haki, amani, utulivu na Umoja wa kitaifa.

Maeneo mengine ni ushiriki wa wanawake na makundi maalumu katika siasa na demokrasia ya vyama vingi vya siasa, Elimu ya Uraia, Rushwa na Maadili katika Siasa na Uchaguzi, Ruzuku ya Serikali kwa Vyama vya Siasa, Uhusiano wa Siasa na Mawasiliano kwa Umma pamoja naKatiba Mpya.

“Hivyo, Kikosi Kazi kinaalika taasisi, kikundi cha watu na mtu yeyote mwenye maoni, mapendekezo au nyaraka kuhusu masuala hayo tisa au mengine yoyote yanayohusu demokrasia ya vyama vingi vya siasa, ambayo anaona yatasaidia Kikosi Kazi kuandaa mapendekezo mazuri na yanayotekelezeka, awasilishe maoni, mapendekezo au nyaraka hizo,” ilisema taarifa hiyo.

Taarifa hiyo imeainisha njia za kuwasilisha maoni hayo kuwa ni pamoja na Barua pepe, taskforcemaoni@orpp.go.tz, ujumbe WhatsApp kwenda kwa Katibu wa Kikosi Kazi kupitia namba 0784 394883, Sanduku la Posta, 2851 Dodoma;

Njia nyingine iliyoainishwa ni kuwasilisha moja kwa moja katika Ofisi za Msajili wa Vyama vya Siasa zilizopo; Dodoma viwanja vya Nanenane Nzuguni, katika Jengo la Wizara ya Kazi, Mtaa wa Nzuguni A; Dar-es Salaam, mtaa wa Shaaban Robert mkabala na Shule ya Msingi Bunge na Zanzibar, mtaa wa Mbweni Matrekta.

Aidha kupitia taarifa hiyo kikosi kazi kimebainisha kuwa pamoja na kukusanya na kupokea maoni kwa njia tajwa hapo juu kinaandaa utaratibu maalumu utakaotumika kukaribisha taasisi, vikundi na watu maalum kuzungumza na...

Habari

  • ZINGATIENI SHERIA, KATIBA NA KANUNI YA VYAMA VYENU - MUTUNGI.
    tokea mwezi 1
  • Political Parties Council Urges Ethical Campaigning, Applauds Government’s Gender Initiatives
    tokea miezi 3
  • Msajili Aipongeza CHADEMA kwa Kuonesha Ukomavu wa Demokrasia Nchini
    tokea miezi 5
  • Tanzia
    tokea miezi 6

Nifanyaje...

  • Kusajili Chama cha Siasa?

Machapisho

  • Taarifa kwa Umma Kuhusu Msimamo wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa dhidi ya CHADEMA
  • KANUNI ZA KURATIBU MIKUTANO YA HADHARA YA VYAMA VYA SIASA YA MWAKA 2023
  • KANUNI ZA KURATIBU MIKUTANO YA HADHARA YA VYAMA VYA SIASA YA MWAKA 2023
  • THE POLITICAL PARTIES AFFAIRS LAWS (AMENDMENT) ACT, 2024
  • ORODHA YA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA 2025

Wasiliana Nasi

  • S.L.P : S.L.P 2851 Dodoma
  • Simu : +255 26 23322500
  • Nukushi : +255 26 2323525
  • Barua Pepe : info@orpp.go.tz
  • Website :https://www.orpp.go.tz

Kurasa za Karibu

  • eOffice
  • Video Mpya
  • Staff Mail
  • Huduma Zetu
  • Vyama Vya Siasa

Tovuti Mashuhuri

  • e-Mrejesho
  • Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tume ya Uchaguzi

Mitandao ya Kijamii

© 2017 Office of Registrar of Political Parties - All Rights Reserved

  • Ramani Ya Tovuti
  • Sera YA Faragha
  • Angalizo