• English
  • Staff Mail
  • Maswali
  • Wasiliana Nasi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa

Tanzania Census 2022
  • Kuhusu sisi
    • Mamlaka
    • Dira
    • Majukumu
    • Muundo
    • Uongozi
    • Historia
  • Shughuli za Ofisi
    • Usajili wa Vyama
    • Uratibu wa Vyama
    • Ufuatiliaji wa Vyama
    • Gharama za Uchaguzi
    • Ruzuku ya Vyama
    • Utatuzi wa Migogoro
    • Taarifa za Vyama vya Siasa
  • Vyama vya Siasa
    • Usajili wa Kudumu
    • Usajili wa Muda
    • Orodha ya Vyama Vya Siasa
    • Baraza la Vyama
  • Sheria na Machapisho
    • Katiba
    • Sera
    • Sheria
    • Kanuni
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu EE
    • Fomu PP
    • Fomu za Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Matangazo
    • Mikutano
    • Warsha
    • Nafasi za kazi
    • Zabuni
  • Ziara
    • Taratibu za Ziara
    • Fomu ya Maombi
    • Utimilifu na Makatazo
    • Maoni ya Watembeleaji

WANASIASA WAACHE PROPAGANDA, WAUSOME VIZURI MUSWADA

Serikali inawaonya Wanasiasa kuacha propaganda za kupindisha ukweli na kutoa tafsiri potofu kuhusu Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 2018 kwa lengo la kuuhadaa umma kukataa muswada bali watumie fursa hii baada ya kuusoma , kutoa maoni yao stahiki kwa lengo la kuuboresha .

Kauli hiyo imetolewa jana Desemba 20, 2018 na Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa Bw. Sisty Nyahozawakati wa mahojiano ya moja kwa moja naBBC Swahili kwenye kipindi chaDira ya Dunia kilichorushwa 20 Desemba 2018 saa tatu usiku.

Akijibu swali lililoulizwa kuhusiana na Msajili wa Vyama vya Siasa kuingilia shughuli za chama cha siasa kwa kumsimamisha mwanachama wa chama cha siasa uanachama, amesema suala hilo halina ukweli wowote bali kifungu kinampa Msajili mamlaka ya kumsimamisha mwanachama wa chama cha siasa kufanya siasa kwa muda utakaowekwa kama atakiuka sheria na si kumsimamisha uanachama.

Nyahoza alisisitiza kuwa malalamiko ya wanasiasa kwa sasa hayana msingi wowote kwa sababu lengo la Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa 2018 ni kuboresha Sheria ya Vyama vya Siasa iliyopo sasa ili kukidhi mahitaji ya wakati huu, kwendana na wakati na pia kuondoa changamoto zilizopo.

“Swala la msingi kwa sasa ni kuwaasa wanasiasa waache kupindisha na kutoa tafsiri potofu kuhusu muswada huo kwa lengo la kuhadaa umma ili wadau/wananchi waukatae muswada bali watumie fursa hii baada ya kuusoma kuwasilisha maoni yao kwenye kamati ya bunge ambayo itakaribisha maoni ya wadau kwa lengo la kuuboresha badala ya kuendekeza propaganda zisizo na tija” aliendelea kusisitiza.

Maoni ya wadau kuhusiana na muswada huu yalianza kukusanywa mwaka 2013 na wadau wakuu ambao ndio vyama vya siasa walishirikishwa kutoa maoni yao. Vyama viliwasilisha maoni yao kwa chama kimoja kimoja na pia kupitia mijadala kwenye vikao vya Baraza la Vyama vya Siasa .

Habari

  • Wadau Waalikwa Kutoa Maoni Yatakayofanyiwa Kazi na Kikosi Kazi cha Mhe. Rais Kuhusu Masuala ya Demokrasia Nchini
    tokea mwezi 1
  • Vyama vya Siasa Kuendeleza Ushirikiano na Serikali, Vyawapongeza Rais Samia, Dkt. Mwinyi
    tokea miezi 10
  • Serikali Yatoa Onyo kwa Vyama vya Siasa Vitakavyoshirikiana Kinyemela Wakati wa Kampeni
    tokea mwaka 1
  • WANASIASA WAACHE PROPAGANDA, WAUSOME VIZURI MUSWADA
    tokea miaka 3

Nifanyaje...

  • Kusajili Chama cha Siasa?

Machapisho

  • Awamu ya Pili ya Ukusanyaji wa Maoni ya Wadau wa Demokrasia ya Vyama Vingi vya Siasa
  • Ratiba ya ukusanyaji wa Maoni ya Wadau wa Demokrasia ya Vyama vingi vya Siasa
  • Marufuku mtu yoyote au taasisi kutumia jina, nembo, rangi na alama ya chama cha siasa cha "Umoja Party" hadi mchakato wa kupata usajili wa muda utakapo kamilika.
  • KUKARIBISHA MAONI YA KUFANYIWA KAZI NA KIKOSI KAZI CHA MHESHIMIWA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
  • Kikosi Kazi cha Kupitia Hoja zilizojitokeza katika Mkutano wa Wadau wa Demokrasia ya Vyama vingi

Wasiliana Nasi

  • S.L.P : S.L.P 2851 Dodoma
  • Simu : +255 26 23322500
  • Nukushi : +255 26 2323525
  • Barua Pepe : info@orpp.go.tz
  • Website :https://www.orpp.go.tz

Kurasa za Karibu

  • eOffice
  • Video Mpya
  • Staff Mail
  • Huduma Zetu
  • Vyama Vya Siasa

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tume ya Uchaguzi

Mitandao ya Kijamii

© 2017 Office of Registrar of Political Parties - All Rights Reserved

  • Ramani Ya Tovuti
  • Sera YA Faragha
  • Angalizo