• English
  • Staff Mail
  • Maswali
  • Wasiliana Nasi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa

  • Kuhusu sisi
    • Mamlaka
    • Dira
    • Majukumu
    • Muundo
    • Uongozi
    • Historia
  • Shughuli za Ofisi
    • Usajili wa Vyama
    • Uratibu wa Vyama
    • Ufuatiliaji wa Vyama
    • Gharama za Uchaguzi
    • Ruzuku ya Vyama
    • Utatuzi wa Migogoro
    • Taarifa za Vyama vya Siasa
  • Vyama vya Siasa
    • Usajili wa Kudumu
    • Usajili wa Muda
    • Orodha ya Vyama Vya Siasa
    • Baraza la Vyama
  • Sheria na Machapisho
    • Katiba
    • Sera
    • Sheria
    • Kanuni
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu EE
    • Fomu PP
    • Fomu za Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Matangazo
    • Mikutano
    • Warsha
    • Nafasi za kazi
    • Zabuni
  • Ziara
    • Taratibu za Ziara
    • Fomu ya Maombi
    • Utimilifu na Makatazo
    • Maoni ya Watembeleaji

Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara

Chama cha siasa ni nini?

Kwa mujibu wa kifungu cha 3 cha Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 1992, Chama cha siasa ni kundi wa watu wenye lengo la kuunda Serikali kupitia uchaguzi halali.

2. Je kuna hatua ngapi katika kusajili chama?

Ndio, kuna hatua mbili. Usajili wa muda na usajili wa kudumu.

3. Je ni nini kinahitajika ili kupata usajili wa muda?

• Wanzilishi wawili watawasilisha maombi ya usajili wa muda kwa kujaza fomu maalumu wakiambatanisha na katiba na kanuni za chama kitarajiwa. • Chama tarajiwa kinatakiwa kutoa uhuru wa mtanzania yoyote kuweza kujiunga bila kuwa na ubaguzi wowote wa kijinsia,kidini, kiitikadi n.k • Kulipa ada ya maombi ya usajili ya shilingi 25,000. • Usajili wa muda utadumu kwa muda wa siku 180, ndani ya muda huo, chama kitatakiwa kutafuta wanachama wasiopungua 2000 ( 200 kwa kila mkoa) katika mikoa 10, mikoa miwili kati ya hiyo ni lazima iwe Tanzania Zanzibar na mkoa mmoja kati ya hiyo miwili, uwe Pemba. • Kutimiza masharti ya usajili wa muda yaliyopo kwenye sheria

4. Je ni nini kinahitajika ili kupata usajili wa kudumu?

• Baada ya kupata wanachama 2000 ndani ya siku 180, Waanzilishi watawasilisha maombi ya usajili wa kudumu kwa kujaza fomu maalumu. • Kulipa ada ya usajili wa kudumu ya shilingi 50,000. • Chama kiwe kimepata Ofisi ya Makao makuu na anuani ya posta kwa ajili ya mawasiliano rasmi na kuchagua viongozi wa kitaifa. • Chama kiwe kimetimiza masharti yote ya kupata usajili wa kudumu yaliyopo kwenye sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 2010 iliyofanyiwa marekebisho 2015.

5. Je chama cha siasa kinaweza kufutwa na kwa nini?

Ndio. Chama cha siasa kinaweza kufutwa iwapo chama hicho kitakiuka masharti ya usajili yaliyopo kwenye Sheria au endapo kitakiuka kifungu chochote cha Sheria ya Vyama vya Siasa ya Mwaka 1992

6. Je kuna hatua zozote hufuatwa wakati wa kukifuta chama cha siasa?

Ndio. Msajili atakitaarifa chama husika nia ya kukifuta kwa maandishi akieleza mapungufu aliyoyabaini. Endapo chama cha siasa kitawasilisha utetezi, Msajili atamutaarifu kwa maandishi Waziri anayeshughulikia mambo ya siasa nia yake ya kutaka kufuta usajili wa chama hicho akiambatanisha na maelezo ya utetezi yaliyotolewa na chama hicho. Kisha Msajili anakitaarifu chama kufutwa kwa usajili kwa fomu maalumu endapo hajaridhika na utetezi wa chama au chama hakijawasilisha utetezi. Kwa mujibu wa sheria ya nyama vya siasa, Msajili wa Vyama vya siasa ndio mwenye maamuzi ya mwisho kuhusu kukifutia chama usajili wake.

Ni vyama vingapi vya siasa ambavyo vimesajiliwa nchini Tanzania

Kuna vyama 19 ambavyo vimesajiliwa venye usajili wa kudumu na chama kimoja chenye usajili wa muda. Bonyeza hapa kuvifahamu

Habari

  • ZINGATIENI SHERIA, KATIBA NA KANUNI YA VYAMA VYENU - MUTUNGI.
    tokea wiki 4
  • Political Parties Council Urges Ethical Campaigning, Applauds Government’s Gender Initiatives
    tokea miezi 3
  • Msajili Aipongeza CHADEMA kwa Kuonesha Ukomavu wa Demokrasia Nchini
    tokea miezi 4
  • Tanzia
    tokea miezi 5

Nifanyaje...

  • Kusajili Chama cha Siasa?

Machapisho

  • Taarifa kwa Umma Kuhusu Msimamo wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa dhidi ya CHADEMA
  • KANUNI ZA KURATIBU MIKUTANO YA HADHARA YA VYAMA VYA SIASA YA MWAKA 2023
  • KANUNI ZA KURATIBU MIKUTANO YA HADHARA YA VYAMA VYA SIASA YA MWAKA 2023
  • THE POLITICAL PARTIES AFFAIRS LAWS (AMENDMENT) ACT, 2024
  • ORODHA YA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA 2025

Wasiliana Nasi

  • S.L.P : S.L.P 2851 Dodoma
  • Simu : +255 26 23322500
  • Nukushi : +255 26 2323525
  • Barua Pepe : info@orpp.go.tz
  • Website :https://www.orpp.go.tz

Kurasa za Karibu

  • eOffice
  • Video Mpya
  • Staff Mail
  • Huduma Zetu
  • Vyama Vya Siasa

Tovuti Mashuhuri

  • e-Mrejesho
  • Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tume ya Uchaguzi

Mitandao ya Kijamii

© 2017 Office of Registrar of Political Parties - All Rights Reserved

  • Ramani Ya Tovuti
  • Sera YA Faragha
  • Angalizo