• English
  • Staff Mail
  • Maswali
  • Wasiliana Nasi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa

Tanzania Census 2022
  • Kuhusu sisi
    • Mamlaka
    • Dira
    • Majukumu
    • Muundo
    • Uongozi
    • Historia
  • Shughuli za Ofisi
    • Usajili wa Vyama
    • Uratibu wa Vyama
    • Ufuatiliaji wa Vyama
    • Gharama za Uchaguzi
    • Ruzuku ya Vyama
    • Utatuzi wa Migogoro
    • Taarifa za Vyama vya Siasa
  • Vyama vya Siasa
    • Usajili wa Kudumu
    • Usajili wa Muda
    • Orodha ya Vyama Vya Siasa
    • Baraza la Vyama
  • Sheria na Machapisho
    • Katiba
    • Sera
    • Sheria
    • Kanuni
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu EE
    • Fomu PP
    • Fomu za Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Matangazo
    • Mikutano
    • Warsha
    • Nafasi za kazi
    • Zabuni
  • Ziara
    • Taratibu za Ziara
    • Fomu ya Maombi
    • Utimilifu na Makatazo
    • Maoni ya Watembeleaji

Rais Samia Awapa Kongole Kikosi Kazi, Aahidi Kufanyiwa Kazi Mapendekezo

Na: Mwandishi Wetu – ORPP

Rais Samia amekipongeza Kikosi Kazi cha kuratibu maoni ya wadau wa demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini kwa kazi nzuri walioifanya ya kuchambua maoni ya wadau kwa kipindi cha miezi 10.

Pongezi hizo zimetolewa leo Ikulu jijini Dar es Salaam wakati akipokea ripoti ya mwisho ya kikosi hicho iliwasilishwa na mwenyekiti wa Kikosi kazi hicho Profesa Rwekaza Mkandala

“Wakati nawapa hii kazi sikujua leo itafika mnikabidhi kitu kilichofanyiwa kazivizuri hivi, kwa hiyo namshukuru Mungu lakini nakushukuruni nanyi na wote mliosaidiana nao katika kazi hii,” alisema Rais Samia.

“lakini la pili niwapongeze kwamba kwa muundo wenu watu kutoka sekta mbalimbali, imani mbalimbali za kisiasa, vyombo vya ulinzi, NGO, vyombo vya habari lakini mmeweza kujipanga na kufanyakazi mkazalisha kitu kizuri ambacho leo mmewasilisha, hongereni sana”.

Rais Samia amesema kuwa pamoja na kuwa kazi hii ilikuwa ngumu lakini kikosi kazi kimefanikiwa kukamilisha kazi hii ndini ya kipindi cha miezi kumi licha ya kwamba wangeweza kwend hadi zaidi yam waka mmoja kutoka na uzito wake.

Aidha katika pongezi hizo Rais Samia akusita kumshukuru Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Francis Mutungi kwa kutekeleza wajibu wake katika kuhakikisha anaratibu vyema shughuli za kikosi kazi hicho katika kutimiza majukumu yao.

“Katika shukrani nisisahau Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, wakiongozwa na Jaji Mutungi, Jaji Mutungi saa zingine ananipigia simu usiku we mama wee hii kazi uliyonipa nimekwama hapa na hapa, umeaminiwa kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa nenda na kazi yako, ukikwama fedha niambie lakini mengine fanya kazi yako, kwa hiyo nakushukuru umefanya kazi yako na mmefikia pazuri”, alisema Rais Samia.

Katika hatua nyingine Rais Samia amesema kuwa Serikali imepokea ripoti ya kikosi kazi ambapo Serikali inajipanga kupitia mapendekezo hayo kupitia vikosi kadhaa vitakavyongalia mambo kadhaa yanayohitaji wataalamu hususan yanayohusu sheria.

Amesema kuwa Kikosi kazi kimetoa mambo mazuri ambayo serikali kupitia wataalam wake kwa kushirikiana na baadhi ya wajumbe wa kikosi kazi watakaopendekezwa wafanya mapitio ya mapendekezo hayo na kuja na namna bora zaidi ya utekelezaji.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kikosi Kazi cha kuratibu maoni ya wadau wa demeokrasia ya vyama vingi vya siasa, Prof. Rwekaza Mkandara akiwasilisha taarifa ya ripoti yao ametumia fursa hiyo kumpongeza Mhe. Rais Samia pamoja na Rais Dkt. Hussein Ally Mwinyi kwa juhudi zao za za kuwaletea watanzania na wanzanibar maendeleo ya kiuchumi, kisiasa na kijamii hususan kuboresha demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini.

Prof. Mukandala amesema kuwa Kikosi kazi hicho kilizinduliwa rasmi mnamo tarehe tarehe 11 Januari 2022 na mpaka sasa kimefanya kazi zifuatazo: kupitia hadidu za rejea, kuchambua hotuba za kufungua na kufunga mkutan...

Habari

  • Rais Samia Awapa Kongole Kikosi Kazi, Aahidi Kufanyiwa Kazi Mapendekezo
    tokea miezi 5
  • RAMBIRAMBI
    tokea miezi 7
  • Wadau Waalikwa Kutoa Maoni Kikosi Kazi cha Rais
    tokea miezi 11
  • Vyama vya Siasa Kuendeleza Ushirikiano na Serikali, Vyawapongeza Rais Samia, Dkt. Mwinyi
    tokea mwaka 1

Nifanyaje...

  • Kusajili Chama cha Siasa?

Machapisho

  • Utaratibu wa Usajili wa Vyama vya Siasa
  • ORODHA YA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA
  • Awamu ya Pili ya Ukusanyaji wa Maoni ya Wadau wa Demokrasia ya Vyama Vingi vya Siasa
  • Ratiba ya ukusanyaji wa Maoni ya Wadau wa Demokrasia ya Vyama vingi vya Siasa
  • Marufuku mtu yoyote au taasisi kutumia jina, nembo, rangi na alama ya chama cha siasa cha "Umoja Party" hadi mchakato wa kupata usajili wa muda utakapo kamilika.

Wasiliana Nasi

  • S.L.P : S.L.P 2851 Dodoma
  • Simu : +255 26 23322500
  • Nukushi : +255 26 2323525
  • Barua Pepe : info@orpp.go.tz
  • Website :https://www.orpp.go.tz

Kurasa za Karibu

  • eOffice
  • Video Mpya
  • Staff Mail
  • Huduma Zetu
  • Vyama Vya Siasa

Tovuti Mashuhuri

  • Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tume ya Uchaguzi

Mitandao ya Kijamii

© 2017 Office of Registrar of Political Parties - All Rights Reserved

  • Ramani Ya Tovuti
  • Sera YA Faragha
  • Angalizo