RAMBIRAMBI

Nimepokea taarifa ya msiba wa Ndugu Augustino Lyatonga Mrema, aliyekuwa Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha TLP mpaka wakati wa umauti wake kwa masikitiko makubwa. Natoa pole kwa familia ya marehemu Mrema, viongozi na wanachama wa TLP na wote walioguswa na msiba huo. Mwenyezi Mungu aiweke roho yake mahala pema peponi - Jaji F.S.K.Mutungi, Msajili wa Vyama vya Siasa.