Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi akifafanua jambo wakati wa Kikao cha Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria yapitisha makadirio ya mapato na matumizi ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2026/27. Kikao hicho kimefanyika jana tarehe 23 Machi, 2026 katika Ofisi za Bunge jijini Dodoma.
Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa (DRPP), Mhe. Mohammed Ally Ahmed akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha kuhusu marejesho ya gaharama za uchaguzi kwa viongozi wa Vyama vya Siasa vilivyoshiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 warsha hiyo imefanyika leo tarehe 10 Machi 2026 katika Ukumbi wa Mikutano Karimjee jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa, Mhe. Juma Ali Khatibu na kulia ni Kaimu Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa anayeshughulikia Uchaguzi na Misaada, Bw. Fadhili Sultan.
Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji(Mstaafu) Francis Mutungi akiwa katika mazungumzo na Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja Mataifa katika Umoja wa Afrika(UNOAU) Bw. Parfait Onanga-Anyanga alipotembelea Ofisi za Msajili zilizopo Mtaa wa Shaban Robert jijini Dar es Salaam leo tarehe 10 Machi, 2026.
Msajili wa Vyama vya Siasa, Mheshimiwa Jaji Francis Mutungi amefanya mazungumzo ya kikazi na Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Camilius Wambura leo Tarehe 02 February, 2026 katika Ofisi ya IGP jijini Dar es Salaam.
Msajili wa Vyama vya Siasa, Mhe. Jaji Francis Mutungi akizungumza na washiriki wakati wa mafunzo kuhusu Sheria ya Gharama za Uchaguzi kwa viongozi wa kitaifa wa vyama vya siasa yaliyofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam, leo tarehe 18 Agosti 2025.
Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Francis S. K. Mutungi atembelea Banda la Ofisi ya Waziri Mkuu katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa Sabasaba leo tarehe 5 Julai 2025 jijini Dar es Salaam.
Msajili wa Vyama vya Siasa (RPP), Mhe. Jaji Francis Mutungi akifungua Mkutano wa Viongozi wa Vyama vya Siasa ulioandaliwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) uliofanyika leo tarehe 2 Juni, 2025 katika ukumbi wa Mikutano wa Multifunctional – Confusious
Mwezeshaji wa mada kuhusu Sera ya usawa wa kijinsia kutoka Shirika lisilo la Kiserikali la WiLDAF, Dkt. Deus Kibamba akiwasilisha mada wakati wa siku ya pili ya kikao cha Baraza la Vyama vya Siasa kilichofanyika leo tarehe 15 Mei, 2025 mjini Morogoro.
Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, akibadilishana mawazo na Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, Dkt. Emmanuel Mkilia (kushoto) kabla ya kuanza kikao cha Baraza la Vyama vya Siasa tarehe 14 Mei,2025 mjini Morogoro
Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa Ndg. Mohammed Ali Ahmed akizungumza wakati wa kufunga mafunzo ya viongozi wa vyama vya siasa leo tarehe 6 Mei, 2025 yaliokuwa yakifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hazina jijini Dar es Salaam.