• English
  • Staff Mail
  • Maswali
  • Wasiliana Nasi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa

  • Kuhusu sisi
    • Mamlaka
    • Dira
    • Majukumu
    • Muundo
    • Uongozi
    • Historia
  • Shughuli za Ofisi
    • Usajili wa Vyama
    • Uratibu wa Vyama
    • Ufuatiliaji wa Vyama
    • Gharama za Uchaguzi
    • Ruzuku ya Vyama
    • Utatuzi wa Migogoro
    • Taarifa za Vyama vya Siasa
  • Vyama vya Siasa
    • Usajili wa Kudumu
    • Usajili wa Muda
    • Orodha ya Vyama Vya Siasa
    • Baraza la Vyama
  • Sheria na Machapisho
    • Katiba
    • Sera
    • Sheria
    • Kanuni
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu EE
    • Fomu PP
    • Fomu za Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Matangazo
    • Mikutano
    • Warsha
    • Nafasi za kazi
    • Zabuni
  • Ziara
    • Taratibu za Ziara
    • Fomu ya Maombi
    • Utimilifu na Makatazo
    • Maoni ya Watembeleaji

Msajili Aipongeza CHADEMA kwa Kuonesha Ukomavu wa Demokrasia Nchini

Habari na: ORPP

Msajili wa Vyama vya Siasa amekipongeza Chama cha CHADEMA kwa kudumisha Demokrasia nchini. Pongezi hizo ziliwasilishwa na Msajili Msaidizi Usajili na Ufuatiliaji wa Vyama vya Siasa, Ndg. Sisty Nyahoza alipokuwa akimwakilisha Msajili wa Vyama vya Siasa, Mhe. Jaji Francis Mutungi katika Mkutano Mkuu wa chama hicho uliofanyika tarehe 21 Januari 2025 katika Ukumbi wa Mikutano Mlimani City, jijini Dar es Salaam.

Nyahoza alisema, jukumu la Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa ni kuhudhuria mikutano mikuu ili kuhakikisha chaguzi na teuzi zinazofanywa zinafanyika kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa Sura 278 na Kanuni za Vyama vya Siasa, lengo kuu ikiwa ni kuhakikisha demokrasia nchini inadumishwa na vyama vya siasa vinazingatia Sheria za nchi na Kanuni zake kwa kuwa vyama vya siasa ni Taasisi za umma. Aliendelea kusema, Mhe. Mwenyekiti, Aikaeli Mbowe nikupongeze umeonyesha ukomavu wa wazi wa kidemokrasia. Alimalizia kwa kusema, kwa namna ambavyo mambo yanavyoendelea, ni wazi kuwa chama hicho kimeelewa dhana ya 4R za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa, Mhe. Juma Khatibu akizungumza katika Mkutano huo kwa niaba ya vyama vyote vya siasa nchini ambavyo vilialikwa, alisema Mkutano huu ni muhimu kwa CHADEMA na alitoa rai kuwa utafanyika kwa amani ili kuendelea kudumisha umoja na mshikamo miongoni mwa wanasiasa nchini. Na vyama vya siasa vimesema viko pamoja na CHADEMA katika kipindi hiki cha uchaguzi, hivyo niwatakieni kheri mmalize salama mkutano wenu na kudumisha umoja, alimaliza.

CHADEMA inafanya Mkutano Mkuu ikiwa ni kutimiza takwa la Sheria ya Vyama vya Siasa, na Katiba yake, sambamba na Kanuni walizojiwekea ambapo pamoja na Mkutano huo ambao ni wa Uchaguzi wa Viongozi wa Kitaifa kwa ngazi za Mwenyekiti Taifa, Makamu Mwenyekiti Bara na Zanzibar na Wajumbe wa Kamati Kuu ya Chama hicho ulitanguliwa na chaguzi za Mabaraza ya chama hicho ngazi ya Taifa pia.

Habari

  • ZINGATIENI SHERIA, KATIBA NA KANUNI YA VYAMA VYENU - MUTUNGI.
    tokea siku 5
  • Political Parties Council Urges Ethical Campaigning, Applauds Government’s Gender Initiatives
    tokea miezi 2
  • Msajili Aipongeza CHADEMA kwa Kuonesha Ukomavu wa Demokrasia Nchini
    tokea miezi 3
  • Tanzia
    tokea miezi 5

Nifanyaje...

  • Kusajili Chama cha Siasa?

Machapisho

  • KANUNI ZA KURATIBU MIKUTANO YA HADHARA YA VYAMA VYA SIASA YA MWAKA 2023
  • KANUNI ZA KURATIBU MIKUTANO YA HADHARA YA VYAMA VYA SIASA YA MWAKA 2023
  • THE POLITICAL PARTIES AFFAIRS LAWS (AMENDMENT) ACT, 2024
  • ORODHA YA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA 2025
  • MUUNDO WA TAASISI

Wasiliana Nasi

  • S.L.P : S.L.P 2851 Dodoma
  • Simu : +255 26 23322500
  • Nukushi : +255 26 2323525
  • Barua Pepe : info@orpp.go.tz
  • Website :https://www.orpp.go.tz

Kurasa za Karibu

  • eOffice
  • Video Mpya
  • Staff Mail
  • Huduma Zetu
  • Vyama Vya Siasa

Tovuti Mashuhuri

  • e-Mrejesho
  • Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tume ya Uchaguzi

Mitandao ya Kijamii

© 2017 Office of Registrar of Political Parties - All Rights Reserved

  • Ramani Ya Tovuti
  • Sera YA Faragha
  • Angalizo