• English
  • Staff Mail
  • Maswali
  • Wasiliana Nasi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa

  • Kuhusu sisi
    • Mamlaka
    • Dira
    • Majukumu
    • Muundo
    • Uongozi
    • Historia
  • Shughuli za Ofisi
    • Usajili wa Vyama
    • Uratibu wa Vyama
    • Ufuatiliaji wa Vyama
    • Gharama za Uchaguzi
    • Ruzuku ya Vyama
    • Utatuzi wa Migogoro
    • Taarifa za Vyama vya Siasa
  • Vyama vya Siasa
    • Usajili wa Kudumu
    • Usajili wa Muda
    • Orodha ya Vyama Vya Siasa
    • Baraza la Vyama
  • Sheria na Machapisho
    • Katiba
    • Sera
    • Sheria
    • Kanuni
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu EE
    • Fomu PP
    • Fomu za Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Matangazo
    • Mikutano
    • Warsha
    • Nafasi za kazi
    • Zabuni
  • Ziara
    • Taratibu za Ziara
    • Fomu ya Maombi
    • Utimilifu na Makatazo
    • Maoni ya Watembeleaji

VYAMA VYA SIASA NA WADAU WAKUMBUSHWA KUZINGATIA MATAKWA YA SHERIA YA GHARAMA ZA UCHAGUZI

Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Mhe. Jaji Francis S.K. Mutungi amevikumbusha Vyama vya Siasa na Umma kwa ujumla kuhusu utekelezaji wa matakwa ya Sheria ya Gharama za uchaguzi.

Hayo ameyasema kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyotolewa Julai 17, 2018 ikiwa ni maandalizi ya tukielekea kwenye uchaguzi mdogo wa Jimbo la Buyungu na kata 77 utakaofanyika tarehe 12 Agosti, 2018.

Jaji Mutungi amesema kuwa Sheria ya Gharama za uchaguzi inamtaka kila Mgombea wa Ubunge na Udiwani kuweka wazi mapato na matumizi ya gharama anazotarajia kuzitumia wakati wa uchaguzi husika kwa kujaza fomu maalumu ( EE1 & EE2) ambazo hujazwa na kuwasilishwa kwenye mamlaka husika ndani ya siku saba, kuanzia siku ya uteuzi wa wagombea. Hivyo anasisitiza ujazaji sahihi wa fomu hizo maalumu ili kukidhi matakwa ya Sheria.

Pia, Jaji Mutungi amewataka wagombea, vyama vya siasana umma kwa ujumlakuepuka kufanya vitendo vinavyokatazwa na Sheria za nchi hususani Kanuni za Maadili ya Vyama vya Siasa, Sheria ya Vyama vya Siasa na Sheria ya Gharama za Uchaguzi ili kuhakikisha kuwa uchaguzi unakuwa huru na wa haki na pia unaendeshwa katika hali ya Amani na utulivu.

Sheria ya Gharama ya uchaguzi ni Sheria inayosimamia mapato na matumizi ya fedha zote ambazo zinatarajiwa kutumika na ambazo zimetumika kwa ajili ya uteuzi, kampeni za uchaguzi na shughuli za uchaguzi kwa chama cha siasa, mgombea, Asasi na Serikali. Sheria hii ilianzishwa mwaka 2010 ikiwa na lengo la kudhibiti matumizi ya gharama za uchaguzi na vitendo vinavyokatazwawakati wa mchakato wa uteuzi, kampeni na uchaguzi na pia kuweka uwanja sawa wa kisiasa miongoni wa vyama vya siasa.

Habari

  • ZINGATIENI SHERIA, KATIBA NA KANUNI YA VYAMA VYENU - MUTUNGI.
    tokea mwezi 1
  • Political Parties Council Urges Ethical Campaigning, Applauds Government’s Gender Initiatives
    tokea miezi 3
  • Msajili Aipongeza CHADEMA kwa Kuonesha Ukomavu wa Demokrasia Nchini
    tokea miezi 5
  • Tanzia
    tokea miezi 6

Nifanyaje...

  • Kusajili Chama cha Siasa?

Machapisho

  • Taarifa kwa Umma Kuhusu Msimamo wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa dhidi ya CHADEMA
  • KANUNI ZA KURATIBU MIKUTANO YA HADHARA YA VYAMA VYA SIASA YA MWAKA 2023
  • KANUNI ZA KURATIBU MIKUTANO YA HADHARA YA VYAMA VYA SIASA YA MWAKA 2023
  • THE POLITICAL PARTIES AFFAIRS LAWS (AMENDMENT) ACT, 2024
  • ORODHA YA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA 2025

Wasiliana Nasi

  • S.L.P : S.L.P 2851 Dodoma
  • Simu : +255 26 23322500
  • Nukushi : +255 26 2323525
  • Barua Pepe : info@orpp.go.tz
  • Website :https://www.orpp.go.tz

Kurasa za Karibu

  • eOffice
  • Video Mpya
  • Staff Mail
  • Huduma Zetu
  • Vyama Vya Siasa

Tovuti Mashuhuri

  • e-Mrejesho
  • Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tume ya Uchaguzi

Mitandao ya Kijamii

© 2017 Office of Registrar of Political Parties - All Rights Reserved

  • Ramani Ya Tovuti
  • Sera YA Faragha
  • Angalizo