VYAMA VYA SIASA KUJENGEWA UWEZO UANDAAJI SERA ZA JINSIA NA UTUNZAJI WA REJESTA ZA VIONGOZI WA VYAMA
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kwa kushirikiana na Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Barani Africa (WILDAF), ipo katika mchakato wa kuvijengea uwezo vyama vya siasa kuhusu masuala ya sera za jinsia, uundaji wa madawati ya jinsia ili vikidhi matakwa ya Sheria ya Vyama vya Siasa iliyofanyiwa marekebisho Mwaka 2024, sera ya jinsia na sheria zingine za nchi.