• English
  • Staff Mail
  • Maswali
  • Wasiliana Nasi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa

  • Kuhusu sisi
    • Mamlaka
    • Dira
    • Majukumu
    • Muundo
    • Uongozi
    • Historia
  • Shughuli za Ofisi
    • Usajili wa Vyama
    • Uratibu wa Vyama
    • Ufuatiliaji wa Vyama
    • Gharama za Uchaguzi
    • Ruzuku ya Vyama
    • Utatuzi wa Migogoro
    • Taarifa za Vyama vya Siasa
  • Vyama vya Siasa
    • Usajili wa Kudumu
    • Usajili wa Muda
    • Orodha ya Vyama Vya Siasa
    • Baraza la Vyama
  • Sheria na Machapisho
    • Katiba
    • Sera
    • Sheria
    • Kanuni
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu EE
    • Fomu PP
    • Fomu za Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Matangazo
    • Mikutano
    • Warsha
    • Nafasi za kazi
    • Zabuni
  • Ziara
    • Taratibu za Ziara
    • Fomu ya Maombi
    • Utimilifu na Makatazo
    • Maoni ya Watembeleaji

WAJUMBE WA BODI ZA WADHAMINI ZA VYAMA VYA SIASA WAFUNDWA

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imekutana na wajumbe wa Bodi za Wadhamini za Vyama vya Siasa katika kikao kilichofanyika leo siku ya Jumanne ya tarehe 29 Mei, 2018 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ndogo za Bunge Jijini Dar es salaam, kilichokuwa na lengo la kuwajengea uwezo wajumbe hao katika kutekeleza ipasavyo Sheria ya Vyama vya Siasa katika mapato na matumizi ya vyama vyao .

Akifungua kikao hicho, Bw.Sisty Nyahoza ambaye ni Msajili Msaidizi akimwakilisha Msajili wa Vyama vya Siasa Mhe. Jaji Francis Mutungi, amewaalika wajumbe kushiriki kikamilifu katika kikao hicho ili kuleta tija iliyokusudiwa.

Wakati wa kikao hicho, mada mbalimbali zimewasilishwa zikiwemo mada kuhusu wajibu wa Chama cha Siasa kutunza na kuwasilisha kwa Msajili wa Vyama vya Siasa taarifa za mapato na matumizi ambayo imewasilishwa na Msajili Msaidizi wa Vyamavya Siasa Bw. Sisty Nyahoza .

Mada zingine zilizowasilishwa ni pamoja na mada kuhusu Wajibu wa Bodi za Wadhamini wa Vyama vya Siasa katika masuala ya fedha ambayo imewasilishwa na Bw. Eliuzeus Kalugendo ambaye ni mwakilishi kutoka Ofisi ya Mhasibu Mkuu wa Serikali (ACGEN).

Na mada kuhusu wajibu na majukumu ya wadhamini iliwasilishwa Bw. Joseph Mwakatobe, mwakilishi kutoka Ofisi ya Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA).

Wajumbe pia wamepata fursa ya kuelimishwa kuhusu majukumu ya Bodi za Wadhamini wa Vyama vya Siasa katika ukaguzi wa hesabu za chama, mada iliyowasilishwa na Bw.Benja Majura, mwakilishi kutoka Ofisi ya Taifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (NAO).

Kikao hicho ni moja kati ya jitihada za Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kuhakikisha vyama vya siasa vinatekeleza ipasavyo Sheria ya Vyama vya Siasa na hasa kuhusu masuala ya mapato na matumizi ya vyama vya siasa, ili kuimarisha demokrasia ya vyama vingi nchini.

Habari

  • ZINGATIENI SHERIA, KATIBA NA KANUNI YA VYAMA VYENU - MUTUNGI.
    tokea mwezi 1
  • Political Parties Council Urges Ethical Campaigning, Applauds Government’s Gender Initiatives
    tokea miezi 3
  • Msajili Aipongeza CHADEMA kwa Kuonesha Ukomavu wa Demokrasia Nchini
    tokea miezi 5
  • Tanzia
    tokea miezi 6

Nifanyaje...

  • Kusajili Chama cha Siasa?

Machapisho

  • Taarifa kwa Umma Kuhusu Msimamo wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa dhidi ya CHADEMA
  • KANUNI ZA KURATIBU MIKUTANO YA HADHARA YA VYAMA VYA SIASA YA MWAKA 2023
  • KANUNI ZA KURATIBU MIKUTANO YA HADHARA YA VYAMA VYA SIASA YA MWAKA 2023
  • THE POLITICAL PARTIES AFFAIRS LAWS (AMENDMENT) ACT, 2024
  • ORODHA YA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA 2025

Wasiliana Nasi

  • S.L.P : S.L.P 2851 Dodoma
  • Simu : +255 26 23322500
  • Nukushi : +255 26 2323525
  • Barua Pepe : info@orpp.go.tz
  • Website :https://www.orpp.go.tz

Kurasa za Karibu

  • eOffice
  • Video Mpya
  • Staff Mail
  • Huduma Zetu
  • Vyama Vya Siasa

Tovuti Mashuhuri

  • e-Mrejesho
  • Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tume ya Uchaguzi

Mitandao ya Kijamii

© 2017 Office of Registrar of Political Parties - All Rights Reserved

  • Ramani Ya Tovuti
  • Sera YA Faragha
  • Angalizo