• English
  • Staff Mail
  • Maswali
  • Wasiliana Nasi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa

  • Kuhusu sisi
    • Mamlaka
    • Dira
    • Majukumu
    • Muundo
    • Uongozi
    • Historia
  • Shughuli za Ofisi
    • Usajili wa Vyama
    • Uratibu wa Vyama
    • Ufuatiliaji wa Vyama
    • Gharama za Uchaguzi
    • Ruzuku ya Vyama
    • Utatuzi wa Migogoro
    • Taarifa za Vyama vya Siasa
  • Vyama vya Siasa
    • Usajili wa Kudumu
    • Usajili wa Muda
    • Orodha ya Vyama Vya Siasa
    • Baraza la Vyama
  • Sheria na Machapisho
    • Katiba
    • Sera
    • Sheria
    • Kanuni
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu EE
    • Fomu PP
    • Fomu za Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Matangazo
    • Mikutano
    • Warsha
    • Nafasi za kazi
    • Zabuni
  • Ziara
    • Taratibu za Ziara
    • Fomu ya Maombi
    • Utimilifu na Makatazo
    • Maoni ya Watembeleaji

OFISI YA MSAJILI VYAMA VYA SIASA YAPONGEZWA UENDESHAJI ZOEZI LA UHAKIKI WA VYAMA VYA SIASA

Na: Frank Shija, ORPP

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imepongezwa kwa namna ambavyo imekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha Vyama vya Siasa vinajiendesha kama taasisi na kwa kuzingatia sheria na taraatibu za kidemokrasia.

Pongezi hizo zimetolewa na Katibu Mkuu wa Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC), Ndg. Doyo Hassan Doyo wakati akitoa shukrani mbele ya wawakilishi kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa walipofika katika Ofisi za Makao Makuu ya ADC zilizopo Ilala, Buguruni Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya zoezi la uhakiki wa vyana vya siasa mapema karibu

“Wengine tunapata elimu kupitia dodoso hizi hata katika uendeshaji masuala yetu binafsi mbali na shughuli za chama hivyo zoezi hili limekuwa msaada mkubwa sana kwetu hali inayofanya tuendelee kuwajibika kama mnavyoona”, alisema Doyo.

Doyo aliongeza kuwa kutokana na elimu wanayoipata kupitia zoezi la uhakiki inaonyesha Dhahiri kwamba vyama vya siasa vinatakiwa kuongeza ufanisi zaidi kiatika namna ya kujiendesha kama taasisi ya umma ambapo gharama zinahitajika katika kufanikisha hilo.

“Menejimenti kuiendesha ni gharama hili bado tunasisitiza wenzetu mlione kama Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kuhusu mgao wa ruzuku kwa Vyama vya siasa muangalie namna ya kutubusti nadhani mnaona namna ambavyo tunajiendesha kwa matatizo kama haya ya kudaiwa kodi” alisisitiza Doyo.

Hata hivyo amesema kuwa sisi kama chama tumenufaika pakubwa sana kupitia Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kutokana na viongozi wetu mbalimbali kujengewa uwezo kupitia semina mbalimbali zilizoandaliwa na Ofisi ya Msajili.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Sheria Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa Muhidin Mapeyo ametoa pongezi hizo kwa Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC) kwa namna ambavyo wamejitahidi kurekebisha pale ambapo mapungufu yalibainika wakati wa zoezi la uhakiki lililopita.

“ Vitu vingi ambavyo tulikuwa tunavihitji vimefanywa na tena kwa ubora na ubora uliokuwa unahitajika, kwa hiyo nimpongeze sana Katibu Mkuu kwa mgawanyo wa majukumu pongezi hizi pia zimfikie Mwenyekiti wa chama kwa kazi nzuri mnayoifanya” alisema Mapeyo.

Mapeyo aliongeza kuwa zoezi la uhkaiki limekuwa na tija sana kwa ustawi wa Vyama vya Siasa kwani kupitia zoezi hili vyama vya siasa vimezidi kuimarika hali inayopelekea hata kuongezeka kwa ufanisi katika namna ya utunzaji wa hesabu zao na kupelekea kupungua kwa hati chafu za Mkaguzi wa Hesabu za Serikali

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa inaendelea na zoezi la ukakiki wa vyama vya siasa nchinilililoanza tarehe 29 April 2014 jijini Dar es Salaam ambapo linahusisha Ofisi za Makao Makuu ya Vyama vyote kwa Pnade zote mbili za Muungano kwa maana ya Tanzania Bara na Zanzibar na linatarajiwa kuhitimishwa tarehe 28 Mei 2024 jijini Dodoma, mpaka sasa jumla ya vyama nane vimekwisha hakikiwa am...

Habari

  • ZINGATIENI SHERIA, KATIBA NA KANUNI YA VYAMA VYENU - MUTUNGI.
    tokea mwezi 1
  • Political Parties Council Urges Ethical Campaigning, Applauds Government’s Gender Initiatives
    tokea miezi 3
  • Msajili Aipongeza CHADEMA kwa Kuonesha Ukomavu wa Demokrasia Nchini
    tokea miezi 5
  • Tanzia
    tokea miezi 6

Nifanyaje...

  • Kusajili Chama cha Siasa?

Machapisho

  • Taarifa kwa Umma Kuhusu Msimamo wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa dhidi ya CHADEMA
  • KANUNI ZA KURATIBU MIKUTANO YA HADHARA YA VYAMA VYA SIASA YA MWAKA 2023
  • KANUNI ZA KURATIBU MIKUTANO YA HADHARA YA VYAMA VYA SIASA YA MWAKA 2023
  • THE POLITICAL PARTIES AFFAIRS LAWS (AMENDMENT) ACT, 2024
  • ORODHA YA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA 2025

Wasiliana Nasi

  • S.L.P : S.L.P 2851 Dodoma
  • Simu : +255 26 23322500
  • Nukushi : +255 26 2323525
  • Barua Pepe : info@orpp.go.tz
  • Website :https://www.orpp.go.tz

Kurasa za Karibu

  • eOffice
  • Video Mpya
  • Staff Mail
  • Huduma Zetu
  • Vyama Vya Siasa

Tovuti Mashuhuri

  • e-Mrejesho
  • Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tume ya Uchaguzi

Mitandao ya Kijamii

© 2017 Office of Registrar of Political Parties - All Rights Reserved

  • Ramani Ya Tovuti
  • Sera YA Faragha
  • Angalizo