• English
  • Staff Mail
  • Maswali
  • Wasiliana Nasi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa

  • Kuhusu sisi
    • Mamlaka
    • Dira
    • Majukumu
    • Muundo
    • Uongozi
    • Historia
  • Shughuli za Ofisi
    • Usajili wa Vyama
    • Uratibu wa Vyama
    • Ufuatiliaji wa Vyama
    • Gharama za Uchaguzi
    • Ruzuku ya Vyama
    • Utatuzi wa Migogoro
    • Taarifa za Vyama vya Siasa
  • Vyama vya Siasa
    • Usajili wa Kudumu
    • Usajili wa Muda
    • Orodha ya Vyama Vya Siasa
    • Baraza la Vyama
  • Sheria na Machapisho
    • Katiba
    • Sera
    • Sheria
    • Kanuni
    • Miongozo
    • Taarifa
    • Fomu EE
    • Fomu PP
    • Fomu za Fedha
  • Kituo cha Habari
    • Habari
    • Hotuba
    • Picha
    • Video
    • Taarifa kwa Umma
  • Matangazo
    • Mikutano
    • Warsha
    • Nafasi za kazi
    • Zabuni
  • Ziara
    • Taratibu za Ziara
    • Fomu ya Maombi
    • Utimilifu na Makatazo
    • Maoni ya Watembeleaji

JAJI MUTUNGI ATOA SALAMU ZA POLE KWA FAMILIA YA ALIYEKUWA MWENYEKITI WA BARAZA LA VYAMA VYA SIASA

Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Mhe. Jaji Francis S. K Mutungi leo amefika nyumbani kwa kaka wa Marehemu Peter Kuga Mziray aliyefariki jana katika hospitali ya Rabininsia Tegeta Jijini Dar es Salaam, na kuwapa pole ndugu, jamaa na marafiki waliofika katika msiba huo.

Akizungumza na kaka wa marehemu Bw. John Mziray, Jaji Mutungi amesema kuwa Marehemu Peter Kuga Mziray ni miongoni wa wanasiasa ambao wametoa mchango katika siasa ya vyama vingi nchini.

Wakati wa uhai wake, Marehemu Peter Kuga Mziray aliwahi kuwa Mwenyekiti wa pili wa Baraza la Vyama vya Siasa kwa vipindi viwili kuanzia mwaka 2012 hadi Novemba, 2016.Aliwahi pia kuwa mwanachama na kiongozi wa ngazi ya kitaifa katika Chama cha Tanzania Labour Party (TLP) na baadaye yeye na wenzake, waliamua kuanzisha chama chao kilichoitwa African Progressive Party of Tanzania (APPT- Maendeleo) tarehe 04 Machi, 2003 ambacho alikuwa Rais Mtendaji wa chama hicho kuanzia kuazishwa kwake hadi kilipofutwa rasmimwaka 2016.

Katika mwaka 2005, Mziray aligombea urais kupitia chama cha APPT – Maendeleo na alikuwa Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, na Kiongozi wa Vyama visivyokuwa na wabunge ndani ya Bunge hilo. Peter Kuga Mziray alizaliwa tarehe 10 Oktoba 1959 wilayani Same, Mkoa wa Kilimanjaro.

Habari

  • ZINGATIENI SHERIA, KATIBA NA KANUNI YA VYAMA VYENU - MUTUNGI.
    tokea mwezi 1
  • Political Parties Council Urges Ethical Campaigning, Applauds Government’s Gender Initiatives
    tokea miezi 3
  • Msajili Aipongeza CHADEMA kwa Kuonesha Ukomavu wa Demokrasia Nchini
    tokea miezi 5
  • Tanzia
    tokea miezi 6

Nifanyaje...

  • Kusajili Chama cha Siasa?

Machapisho

  • Taarifa kwa Umma Kuhusu Msimamo wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa dhidi ya CHADEMA
  • KANUNI ZA KURATIBU MIKUTANO YA HADHARA YA VYAMA VYA SIASA YA MWAKA 2023
  • KANUNI ZA KURATIBU MIKUTANO YA HADHARA YA VYAMA VYA SIASA YA MWAKA 2023
  • THE POLITICAL PARTIES AFFAIRS LAWS (AMENDMENT) ACT, 2024
  • ORODHA YA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA 2025

Wasiliana Nasi

  • S.L.P : S.L.P 2851 Dodoma
  • Simu : +255 26 23322500
  • Nukushi : +255 26 2323525
  • Barua Pepe : info@orpp.go.tz
  • Website :https://www.orpp.go.tz

Kurasa za Karibu

  • eOffice
  • Video Mpya
  • Staff Mail
  • Huduma Zetu
  • Vyama Vya Siasa

Tovuti Mashuhuri

  • e-Mrejesho
  • Utumishi wa Umma
  • Ofisi ya Rais Ikulu
  • Bunge la Tanzania
  • Ofisi ya Waziri Mkuu
  • Tume ya Uchaguzi

Mitandao ya Kijamii

© 2017 Office of Registrar of Political Parties - All Rights Reserved

  • Ramani Ya Tovuti
  • Sera YA Faragha
  • Angalizo